la 8 kwa ajili ya Agasti 24 2019 Maadili na Ushawishi Kukabiliana na dhuluma Matendo ya upendo Vipaumbele vyetu Kuwahudumia wengine Katika tukia ID: 815317
Download The PPT/PDF document "“HAO WALIO WADOGO” Somo" is the property of its rightful owner. Permission is granted to download and print the materials on this web site for personal, non-commercial use only, and to display it on your personal computer provided you do not modify the materials and that you retain all copyright notices contained in the materials. By downloading content from our website, you accept the terms of this agreement.
Slide1
“HAO WALIO WADOGO”
Somo
la 8
kwa
ajili
ya
Agasti
24, 2019
Slide2Maadili
na UshawishiKukabiliana na dhuluma
Matendo ya upendoVipaumbele vyetuKuwahudumia
wengine
Katika
tukia fulani, Petro alitoa muhtasari wa huduma ya Yesu: “Alienda huko na huko akitenda kazi njema na kuponya wote walioonewa na Ibilisi” (Matendo 10:38).Katika hotuba ya Mlimani (Mathayo 5-7), Yesu alitufundisha jinsi raia wa ufalme wa Mbinguni wanavyopaswa kuwa.
Maisha ya Yesu yalikuwa kielelezo cha mafundisho yake. Muhtasari wa Petro kwa huduma yake [Yesu] unaaksi kanuni za ufalme wake.
Slide3“
Heri ninyi […] Ninyi ni chumvi ya
dunia […] Ninyi ni nuru ya
ulimwengu.
”
(
Mathayo 5:11, 13, 14)Hiki ndicho kinachotufanya tuwe heri (furaha): kuwa maskini wa roho, kuomboleza kwa sababu ya dhambi, kutenda wema, kuudhiwa kwa ajili ya haki, wenye rehema, wenye moyo safi, wapatinishi, dhuluma dhidi yetu.MAADILI NA USHAWISHINyingi kati ya sifa hizi zinahusiana na namna tunavyowafanyia wengine.Tunakuwa nuru pale tunapowaangazia wengine kwa maneno yetu na mfano wetu.Ili tuwe chumvi ni lazima tuishi na watu wengine, tukiwashawishi na kuboresha maisha yao.
Slide4“
Wafuasi wa Kristo wanapaswa kuwa nuru kwa ulimwengu; lakini Mungu hawalazimishi
kutumia nguvu ili waangaze. Hajaridhia jitihada binafsi za kuonesha
wema wa
juu
.
Anatamani nafsi zao ziongozwe na kanuni za mbinguni; badaye, kama wataingiliana na ulimwengu, wataitangaza nuru iliyo ndani yao. Uaminifu wao wa subira katika kila tendo la maisha litakuwa nuru.”E.G.W. (The Ministry of Healing, cp. 2, p. 36)
Slide5“
Lakini mimi nawaambia, msishindane na
mtu mwovu; lakini mtu
akupigaye
shavu
la kuume, mgeuzie na la pili.” (Mathayo 5:39)Maisha ya wale waliokuwa wakimsikiliza Yesu hayakuwa rahisi. Wenye nguvu waliwatendea vibaya, wengi walikuwa na madeni na walinyanyaswa na wakopeshaji, askari wa Kirumi walikuwa wakiwalazimisha kufanya kazi bila malipo.KUKABILIANA NA DHULUMANi rahisi kutupiliwa mbali kwa chuki katika mazingira haya. Yesu aliwafundisha kujibu kwa upole, kutowachukia lakini wakionesha huruma kwa wale wasiotaka kubarikiwa.Nyakati nyingi hatuwezi kutoa dhuluma, lakini tunaweza kuchagua namna ya kuzikabili: “Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema.” (Warumi 12:21).
Slide6“
Hebu kila siku tuuwakilishe upendo mkubwa wa Kristo kwa kuwapenda maadui
zetu kama Kristo anavyowapenda. Inatupasa kuiwakilisha neema ya Kristo,
hisia kali za
chuki
zitavunjwa na mioyo halisi ya upendo italetwa. Uongofu mwingi utafuata kuliko ilivyo sasa.”E.G.W. (Medical Ministry, p. 254)
Slide7“
Lakini mimi nawaambia, wapendeni adui zenu, waombeeni
wanaowaudhi.” (Mathayo 5:44)Jirani au adui? Katika wakati huo, Wasamaria
walitazamwa kama maadui za
wayahudi
na kinyume chake.Hata hivyo, Yesu alikitoa kisa halisi cha Msamaria ambaye “alikuwa na huruma” (Lk. 10:33) alipomwona adui yake akiwa mhitaji.MATENDO YA UPENDOUfahamu wa akili wa kuhani na Mlawi: “Kama nitamsaidia mtu huyu, kitatokea nini kwangu?”Ufahamu wa akili wa Msamaria mwema: “Kama sitamsaidia mtu huyu, kitatokea nini kwangu?”Ufahamu wa akili wa raia wa ufalme: Kufikiria juu ya mahitaji ya wengine badala ya mahitaji yao wenyewe.
Slide8“
Shikiria kila fursa ili kushiriki furaha ya wanaokuzunguka, ukiwashirikisha upendo wako. Maneno
ya wema, kuwaonea huruma, kuwapongeza, kupambania mengi, upweke wa mmoja
unakuwa kama
kikombe
cha maji ya baridi kwa nafsi yenye kiu. Neno la uchangamfu, tendo la wema, litaenda mbali kumulika mizigo mizito ya waliolemewa na kuchoka. Ni katika huduma isiyo ya ubinafsi ambapo furaha kamili hupatikana. Na kila neno na tendo la huduma hiyo litaandikwa katika vitabu vya mbinguni kama limetendwa kwa Kristo…Ishi katika mwangaza wa upendo wa Mwokozi. Badaye ushawishi wako utabariki ulimwengu. Acha Roho wa Kristo akutawale. Hebu sheria ya wema iwepo daima
katika midomo yako. Uvumilivu na kutokuwa na ubinafsi unaonyesha maneno na matendo ya wale waliozaliwa upya, ili kuishi maisha mapya ndani ya Kristo.”E.G.W. (Testimonies for the Church, vol. 7, cp. 10, p. 49-50)
Slide9“
Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na
Haki yake, na haya mengine mtazidishiwa.” (
Mathayo 6:33)
Mfano
wa mtu tajiri na Lazaro (Luka 16:19-31), unamtambulisha tajiri aliyebaki kutojali mahitaji ya maskini.Katika maisha, mazingira husika kwa tabia zote yanabaki kutobadilika; lakini katika kifo, kama inavyohukumiwa na Mungu, nafasi zao zilibadilika kwa kasi.VIPAUMBELE VYETUKatika mfano mwingine (Luka 12:13-21), Yesu anamwelezea tajiri mwingine aliyekuwa akihofia juu ya utajiri wake. Alikuwa amejikita zaidi katika maisha haya ya muda tu, na akapoteza uzima wa milele.Mifano hii miwili inafundisha kwamba kitu cha muhimu ni kuutafuta kwanza ufalme wa Mungu. Ni lazima pia tuwashirikishe wengine mibaraka hii ya Mungu.
Slide10“
Mungu anatamani wanaume na wanawake kuishi maisha ya juu. Huyatekeleza maisha yao
, siyo kuwapatia mali, lakini kwa kuboresha nguvu zao za
juu kwa
kuifanya
kazi aliyowakabidhi wanadamu—kazi ya kutafuta na kusaidia mahitaji ya wanadamu wenzao. Mwanadamu afanye kazi siyo kwa maslahi yake mwenyewe lakini kwa maslahi ya kila mmoja, kuwabariki wengine kwa ushawishi wake na matendo ya wema.”E.G.W. (Mind, Character and Personality, vol. 2, cp. 71, p. 645)
Slide11“
Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona
una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?’” (Mathayo
25:37)
Mifano
ya Yesu kuhusu ujio wake wa Mara ya Pili (Mathayo 25) vinatukumbusha juu ya umuhimu wa kujiandaa sisi wenyewe na kuishi kulingana na kanuni za ufalme.Mfano wa kondoo na mbuzi ni kielelezo cha hiki. Kutenda rehema na kuwajali wengine ni sehemu ya mtindo wa maisha ya mwenye haki.Hawapaswi hata kufikiria juu yake. Kwa nyongeza, hawatangazi matendo yao ya wema au kutegemea kupewa malipo.Yesu hupokea matendo tunayoyafanya kuwasaidia walio wahitaji kama vile tumeyafanya kwake mwenyewe: “kadri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.” (Mathayo 25:40)KUWAHUDUMIA WENGINE
Slide12“
Ukweli kama ulivyo kwa Yesu hufaya mengi kwa anayeupokea, na siyo
kwa yeye tu, lakini kwa wote wanaoletwa ndani ya mazingira ya ushawishi
wake… Haangalii
uhalisia
wa sasa; haoneshi tamaa; hana tamaa na sifa za wanadamu. Tumaini lake liko mbinguni, na mnyofu, macho yake yakiwa yamemtazama Yesu. Hutenda haki kwakuwa ni haki, na kwa sababu watendao haki tu ndio watakaoingia katika ufalme wa Mungu. Ni mpole na mnyenyekevu, na anafikiria furaha ya wengine… hana tabia ya ukali na ya kidikteta, kama ya wasio na Mungu; lakini huaksi nuru kutoka mbinguni kuja kwa wanadamu.”E.G.W. (Testimonies for the Church, vol. 5, cp. 68, p. 569)