Somo la 3 kwa ajili ya April 18 2020 Jinsi gani Yesu aliitumia Biblia Biblia kama mamlaka Biblia kama mwongozo wa maisha Ni sehemu zipi ID: 814887
Download The PPT/PDF document "MTAZAMO WA YESU NA MITUME KWA BIBLIA" is the property of its rightful owner. Permission is granted to download and print the materials on this web site for personal, non-commercial use only, and to display it on your personal computer provided you do not modify the materials and that you retain all copyright notices contained in the materials. By downloading content from our website, you accept the terms of this agreement.
Slide1
MTAZAMO WA YESU NA MITUME KWA BIBLIA
Somo
la 3
kwa
ajili
ya
April
18, 2020
Slide2Jinsi
gani
Yesu
aliitumia Biblia?Biblia kama mamlakaBiblia kama mwongozo wa maishaNi sehemu zipi za Biblia Yesu alizikubali? Biblia katika ukamilifu wakeBiblia kama historia thabitiJinsi gani mitume waliitumia Biblia?Biblia kama Neno la Mungu
Biblia haikujulikana kama tunavyoijua leo wakati Yesu alipoanza huduma Yake. Agano Jipya lilikuwa bado halijaandikwa.Kwahiyo, tunaweza kusema kwamba Biblia ya Yesu na Mitume ilikuwa ni Agano la Kale. Sehemu hii ya Biblia ilijulikana kama “Maandiko”.Hebu tujifunze namna Yesu na Mitume walivyoyatumia Maandiko, hivyo tutafahamu namna ya kuitumia na kuifahamu Biblia leo.
Slide3BIBLIA KAMA MAMLAKA
“Imeandikwa…”
(
Mathayo
4:4, 7, 10; Luka 4:4, 8, 12)Yesu alijaribiwa na Shetani katika njia maalumu mara kabla ya kuanza huduma Yake. Yesu alijibu kila jaribu kwa nukuu ya Biblia:Biblia ndiyo ilikuwa mamlaka ya juu na msingi imara wa imani ya Yesu.Ni lazima tupokee mwongozo fulani wa Neno la Mungu kabla ya wazo jingine lolote.
Slide4BIBLIA KAMA MWONGOZO WA MAISHA
“
Msidhani
ya
kuwa nalikuja kutangua torati au manabii. La, sikuja kutangua, bali kutimiliza.” (Mathayo 5:17)Yesu aliyaona Maandiko kama mwongozo ambao utatuongoza katika maisha haya.Hakuwa anatoa maelekezo mapya anaposema “Bali mimi nawambieni
” (Mt. 5:22, 28, 32, 39, 44). Alikuwa akifafanua kile Musa na manabii walichokiandika na kukielezea maana yake halisi.
Pale Yesu
alipoulizwa ni
ipi
iliyo amri
kuu (
Mathayo 22:36-40), alijibu
kwa Maandiko
tena
:
Kumbukumbu
La
Torati
6:5
na
Walawi
19:18.
Agano
Jipya
ni
mwendelezo
,
ufafanuzi
na
utimilizaji
wa
Agano
la Kale.
Linaelezea
Agano
la Kale
katika
nuru
ya
kifo
,
ufufuo
na
utukufu
wa
Yesu
.
Slide5BIBLIA KATIKA UKAMILIFU WAKE
“Kisha
akawaambia
, ‘Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa na katika manabii na Zaburi.’” (Luka 24:44)Biblia ya Kiebrania (Agano la Kale) ilikuwa na muundo ufuatao:Yesu aliyatazama Maandiko kama yaliyovuviwa. Alifahamu
kwamba yanamamlaka ya kutufundisha mapenzi ya Mungu.Hiki ndicho alichokifundisha, na alichotuamuru kukifundisha (Mathayo 28:20).
Slide6BIBLIA KAMA HISTORIA HALISI
“Tena, palikuwa
na
wenye ukoma wengi katika Israeli zama za nabii Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu” (Luka 4:27)Bali na kuiangalia Biblia iliyo Neno la Mungu na msingi wa kila fundisho na mwongozo wa maisha, Yesu pia aliitazama kama kitabu cha Kihistoria.Alitaja visa vyao kama mfano wa kuufuata au kutoufuata, kama ishara ya nini kilikuwa kinaenda kutokea, au kama chanzo cha fundisho.Yesu alimtaja: Adam na Hawa, Habili, Nuhu, Sodoma na Gomora, mke wa Lutu, Daudi, Sulemani, Eliya, Elisha, Yona, Zekaria, Isaya…
Alirejea watu katika Biblia kama watu halisi walioishi sehemu halisi na walikouwa sehemu ya matukio halisi.
Slide7BIBLIA KAMA NENO LA MUNGU
“Kwa
maana
Maandiko yasema juu ya Farao, ya kwamba, Nilikusimamisha kwa kusudi hili, ili nionyeshe nguvu zangu kwako, jina langu likatangazwe katika nchi yote.’” (Warumi 9:17)Paulo aliitambulisha Biblia kama vile iliyoongea maneno ya Mungu kwa Farao. Mungu anatambuliwa na Andiko hapa, kama ilivyo katika Wagalatia 3:8. Andiko NI Neno la Mungu.Kila mwandishi wa Agano Jipya alilitumia Agano la Kale kama Neno la Mungu. Waliyapokea maneno ya Manabii kwa jinsi
hiyo.Walitumia visa vya watu kama Daudi, Lutu na Ibrahimu kama mifano bora ya kufundishia (Rum. 11:9; 2Pt. 2:7; Yakobo 2:23).Waliufuata mfano wa Yesu, wakiikubali Biblia kama alivyofanya. Ni lazima pia tuikubali Biblia NZIMA kama msingi wa imani na kuamini kwetu.
Slide8“Neno la Mungu linajumuisha
Maandiko ya Agano la Kale pamoja na
Agano
Jipya
. Moja halijakamilika bila jingine. Yesu alitangaza kwamba kweli za Agano la Kale zina thamani sawa na za Agano Jipya…Kristo alijifunua kwa wazee, kama mfano wa ile huduma ya kutoa kafara, kama ilivyoonyeshwa katika torati, na kama ilivyofunuliwa na manabii, ndiye utajiri wa Agano la Kale. Kristo katika maisha Yake, kifo Chake, na kufufuka Kwake, Kristo kama alivyofunuliwa na Roho Mtakatifu, ndiye hazina ya Agano Jipya
. Mwokozi wetu, nuru ya utukufu wa Baba, ni Agano la Kale na Jipya.”E.G.W. (Christ’s Object Lessons, cp. 11, p. 126)